Kaburi la babake Assad lachomwa moto Syria
Wapiganaji wa waasi nchini Syria wamepigwa picha wakiwa wamesimama kando ya kaburi la babake Rais Assad aliyeundolewa madarakani hayati rais Hafez al-Assad.
Sehemu ya kaburi la babake rais aliyepinduliwa wa Syria Bashar al-Assad limechomwa moto.
Babake Assad na mtangulizi wake alifariki mwaka 2000 na alizikwa kwenye kaburi katika kijiji cha mababu wa familia hiyo cha Qardaha.
Kulingana na shirika la kufuatilia vita lenye makao yake nchini Uingereza, waasi wa Syrian Observatory for Human Rights (SOHR) walichoma moto kaburi hilo, lililoko katikati mwa Latakia ya jumuiya ya Alawite ya Assad.
CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES
CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES