Mwanamfalme Harry aliambia BBC kwamba anataka maridhiano na Familia ya Kifalme

Mwanamfalme Harry aliambia BBC kwamba anataka maridhiano na Familia ya Kifalme

Duke wa Sussex ameiambia BBC kuwa “angependa maridhiano” na Familia ya Kifalme, katika mahojiano ya kihisia ambayo alisema “amehuzunishwa” kwa kupoteza changamoto ya kisheria juu ya usalama wake nchini Uingereza.

Mwanamfalme Harry alisema Mfalme “hatazungumza nami kwa sababu ya mambo haya ya usalama”, lakini kwamba hakutaka kupigana tena na “hakujua baba yake ana muda gani”.

Mwanamfalme alizungumza na BBC News huko California baada ya kupoteza kesi ya rufaa kuhusu viwango vya usalama ambavyo yeye na familia yake wanastahili kuwa nazo wakiwa nchini Uingereza.

Ikulu ya Buckingham ilisema: “Maswala haya yote yamechunguzwa mara kwa mara na kwa uangalifu na mahakama, na hitimisho sawa katika kila utaratibu.”

h

CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES

Maelezo ya picha, Harry na Mkewe Meghan, wamekuwa wakiishi Marekani tangu 2020 (picha iyao ilichukuliwa mwezi Aprili)

Baada ya uamuzi wa mahakama ya Ijumaa, Mwanamfalme Harry alisema: “Sioni ulimwengu ambao ningemrudisha mke wangu na watoto wangu Uingereza kwa wakati huu.”

“Kumekuwa na kutoelewana kwingi kati yangu na baadhi ya familia yangu,” aliongeza, lakini sasa “nimewasamehe”.

“Ningependa maridhiano na familia yangu. Hakuna maana kuendelea kupigana tena, maisha ni ya thamani,” alisema Prince Harry, ambaye alisema mzozo juu ya usalama wake “siku zote umekuwa suala muhimu”.

Ufitinema Aime Gerard

Maak 'n opvolg-bydrae

Jou e-posadres sal nie gepubliseer word nie. Verpligte velde word met * aangedui