Tetesi za Soka Ulaya: Aston Villa haina mpango wa kumuuza Rogers
Aston Villa haina mpango wa kumuuza Morgan Rogers huku klabu kadhaa zikiwa na nia ya kumsajili kiungo huyo mshambuliaji, Barcelona bado wana hamu ya kumsajili Marcus Rashford kutoka Manchester United na Real Madrid wanafanya mazungumzo na beki wa kulia wa Inter Milan Denzel Dumfries.
Aston Villa wanajua kuwa kuna nia ya kumsajili kiungo mshambuliaji Morgan Rogers kutoka klabu kadhaa, ikiwemo Arsenal, lakini hawana mpango wa kumuuza mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 23. (Telegraph – subscription required)
Beki wa pembeni wa Eintracht Frankfurt, Nathaniel Brown, mwenye umri wa miaka 22, ndiye anayewindwa na Bayern Munich na Arsenal. (The Athletic – subscription required)
Manchester City na Chelsea wanamtaka beki wa pembeni wa Juventus Andrea Cambiaso, 26, huku Barcelona pia ikifuatilia hali ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Italia. (Gazzetta dello Sport – in Italian)
CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES
Liverpool na Paris St-Germain huenda zote zikamtaka winga wa RB Leipzig Yan Diomande lakini klabu hiyo ya Ujerumani haitikiswi na hali hiyo kwani inaamini mchezaji huyo wa miaka 19 hataendelea kuwa nao kwa mwaka mwingine tu bali pia atasaini mkataba mpya ulioboreshwa. (Sky Sports Germany)
Kocha wa Barcelona Hansi Flick, mkurugenzi wa michezo Deco na rais Joan Laporta bado wana hamu ya kumsajili mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford kwa mkataba wa kudumu huku Bayern Munich, Newcastle, Tottenham na Aston Villa wakimtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 28. (The I)
Juventus wanaangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Bournemouth na Uholanzi Justin Kluivert mwenye umri wa miaka 27 kama mbadala wa mchezaji wa Real Madrid mwenye umri wa miaka 26 wa Morocco Brahim Diaz. (Gazzetta dello Sport – in Italian)
Manchester United wamemfuatilia mlinzi wa Juventus na Ufaransa Pierre Kalulu na klabu ya Turin huenda ikalazimika kumuuza mchezaji huyo wa miaka 25 ili kusawazisha masuala ya miamala baada ya kushindwa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa. (Corriere dello Sport – in Italian)
Kiungo wa kati wa Ureno Mateus Fernandes, 21, ameruhusiwa kuondoka West Ham baada ya mawasiliano kutoka Manchester United na Arsenal, huku Liverpool na Paris St-Germain pia zikimfuatilia. (Teamtalk)
Aston Villa, Atletico Madrid na Borussia Dortmund zinamtaka mshambuliaji wa Club Brugge, Mjerumani Nicolo Tresoldi, 21, baada ya msimu mzuri Ubelgiji. (The Athletic – subscription required)
Real Madrid wamefanya mazungumzo na mlinzi wa Inter Milan Denzel Dumfries, ambaye kima chake cha kuuza ni pauni milioni 21.6, huku wakimwona mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 30 kama shabaha yao kuu ya kuimarisha safu yao ya beki wa kulia. (Athletic)